Mataifa ya Misri na Ivory Coast yamefuzu kushiriki michuano ya Olimpiki 2020, itakayofanyika Tokyo, Japan, baada ya timu zao za taifa chini ya umri wa miaka 23 kutinga hatua ya fainali. Mataifa hayo yametinga hatua ya fainali ya michuano ya Afrika chini ya umri wa miaka 23, inayoendelea nchini Misri, kwa kuzitupa nje Afrika kusini na Ghana. Hata hivyo mshiriki wa tatu kutoka Afrika kwenye michuano ya Olimipiki 2020, anatarajiwa kufahamika baada ya mchezo wa kumsaka mshindi wa tatu na wanne, utakaochezwa kesho kati ya Ghana na Afrika kusini.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |