• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • UN-Habitat yatoa wito kwa wafadhili kutoa fedha za miradi

    (GMT+08:00) 2019-11-21 19:40:50
    Shirika la Umoja wa Mataifa la Makazi (UN-Habitat) limetoa wito kwa nchi wanachama na wafadhili kutoa fedha za kuwezesha kutekeleza miradi.

    Katika Mkutano wa Bodi ya Usimamizi jana,Mkurugenzi Mtendaji wa UN-Habitat Maimuna Shariff alisema Shirika hilo kwa sasa halina fedha za kutekeleza miradi yake.

    Aidha alisema tangu achukue uongozi wa Shirika hilo mapema mwaka jana,alipata shirika hilo likipitia changamoto za kifedha na hivyo kusitisha shughuli za kuwaajiri watu upya.Alisema kufikia sasa kuna nafasi za kazi 34 ambazo hazijajazwa kutokana na uhaba wa fedha.

    Bi Shariff aliyapongeza mataifa ya Kenya na Norwaykwa kuongezea mchango wao kila mwaka.

    Kenya imeongeza mchango wake kutoka Sh70 milioni hadi Sh100 milioni.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako