Rais Donald Trump wa Marekani amesema atatoa rekodi zake za kifedha kabla ya uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka 2020, kama alivyoahidi alipogombea urais mwaka 2016. Mahakama kuu ya nchi hiyo jumatatu ilisimamisha kwa muda uamuzi wa mahakama ya rufaa unaoruhusu kamati ya baraza la wawakilishi la bunge kupata kumbukumbu za miaka nane za kifedha za Trump kutoka kwa kampuni yake ya uhasibu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |