Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu nchini Tanzania imesema itatoa hukumu dhidi ya rais wa zamani wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Jamal Malinzi na wenzake watatu mwezi ujao. Malinzi na wenzake hao wanakabiliwa na mashtaka 20 yakiwemo kula njama, kughushi, kijipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na utakatishaji wa fedha kiasi cha sola za kimarekani 173,335.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |