Baada ya Mbwana Samatta kuangushiwa lawama na mashabiki na wadau mbalimbali wa soka kuwa hajitumi anapokuwa na kikosi cha timu ya Taifa Taifa Stars, mchezaji huyo ameshukuru kwa kuelezwa ukweli na mashabiki wake na kusema atalifanyia kazi suala hilo. Amesema watu wengi hawajaridhishwa na kiwango anachocheza akiwa na timu ya taifa, na kuwahakikishia kuwa atajituma zaidi ili aweze kuwa bora zaidi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |