Caleb Ayodi Malweyi amechaguliwa mwenyekiti mpya kuongoza Shirikisho la Soka la Kenya (FKF) Tawi la Nairobi Magharibi baada ya kuwashinda wapinzani watatu kwenye uchaguzi uliofanyika Nyayo Stadium, Nairobi. Caleb aliyekuwa katibu wa tawi hilo alitwaa wadhifa huo kwa kuzoa kura 38 na kuwanyoa wenzake akiwamo aliyekuwa mwenyekiti wake, Bashir Hussein aliyepata kura tano.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |