Wajumbe 45 wa Kamati ya katiba ya Syria wamewasili kwenye ofisi za umoja wa mataifa mjini Geneva, kurejesha mazungumzo yao kuhusu mpangilio mpya wa katiba wa nchi hiyo. Ofisi ya tume maalumu ya Umoja wa Mataifa kuhusu Syria imesema itaendelea na ushirikiano na Kamati ya katiba ya Syria wiki hii. Hata hivyo ofisi hiyo haijataja mambo halisi lakini imesema itahakikisha vyombo vya habari vinaarifiwa kwa juhudi zote.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |