Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa UNEP limetoa ripoti mpya ikionya kuwa, endapo utoaji wa hewa zinazosababisha ongezeko la joto duniani hautapungua kwa asilimia 7.6 kwa mwaka kati ya mwaka 2020 hadi 2030, dunia itapoteza fursa ya kutimiza lengo lake la kudhibiti ongezeko la joto liwe chini ya nyuzi 1.5. Ripoti hiyo pia imesisitiza kuwa, ni hadi utoaji wa hewa hizo utakapopunguzwa kwa zaidi ya mara tano kuliko kiwango sasa, ndipo lengo la kudhibiti ongezeko la joto ndani ya nyuzi 1.5 litakapotimizwa katika miaka 10 ijayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |