Mamlaka ya usimamizi wa mambo ya kibinadamu ya Syria imeripoti kuwa, watu karibu 485 wamekufa kutokana na hali ngumu ya kibinadamu kwenye kambi ya wakimbizi inayomilikiwa na kundi la kikurdi, kaskazini mashariki nchini Syria. Mamlaka hiyo imesema kati ya watu hao wengi ni jamaa wa wapiganaji wa kundi la IS, ambao walikimbilia kambi ya al-Hol kwenye mkoa wa Hasakah.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |