Wakati mechi za mtoani wa Ligi ya Mpira wa Kikapu Mkoa wa Dar es Salaam (RBA) zikianza leo kwenye Uwanja wa Ndani wa Taifa, timu ya JKT imejitoa kushiriki. Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Kikapu mkoa wa Dar es Salaam, Okare Amesu amethibitisha JKT kujitoa kwenye ligi hiyo iliyofikia hatua ya nane bora. JKT imejitoa kwenye ligi hiyo ili kuweza kujiandaa na Ligi ya Mabingwa Afrika (BAL). Amesu amesema, uwakilishi wa JKT katika Ligi hiyo ni mkubwa na unahitaji kuungwa mkono ili wafanya vizuri na kufika mbali katika Ligi ya Mabingwa Afrika.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |