Serikali ya Sudan Kusini imefungua kiwanda cha kuzalisha kawi ya dizeli katika juhudi za kupunguza uchafzi wa mazingira nchini humo .
Serikali imesema kawi hiyo iytasaidia kupunguza uchafuzi wa hewa unaotokana na matumizi ya jenereta hasa mijini.
Zaidi ya nyumba 100,000 zitafaidika na kawi ya mradi huo mpya na serikali inalenga kuzalisha hadi megawati 100 za kawi ya aina hiyo ifikapo mwaka 2021.
Rais Salva Kiir ameutaja mradi huo kama hatua kubwa ya kuelekea maendeleo nchini humo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |