Wanadhimu Wakuu wa Majeshi ya Korea Kusini wamesema, Korea Kaskazini imerusha makombora mawili yasiyotambulika katika Bahari ya Mashariki.
Taarifa iliyotolewa na Wanadhimu hao imesema, makombora hayo yalirushwa kutokea mkoa wa mashariki wa Hamgyong Kusini nchini Korea Kaskazini kuelekea bahari ya Mashariki majira ya saa 10:59 kwa saa za huko.
Jeshi la Korea Kusini limesema, makombora hayo yalirushwa ndani ya sekunde 30, na kuitaka Korea Kaskazini kuacha vitendo hivyo vinavyoongeza mvutanbo wa kijeshi katika Peninsula ya Korea.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |