• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Waandamanaji 31 wauawa katika maandamano ya kuipinga serikali nchini Iraq

    (GMT+08:00) 2019-11-29 09:40:15

    Kamati kuu ya haki za binadamu ya Iraq imesema kuwa waandamanaji 31 wameuawa na wengine zaidi ya elfu moja wamejeruhiwa katika siku tatu zilizopita za maandamano ya kuipinga serikali yaliyofanyika huko Baghdad na majimbo ya kusini nchini humo. Mapema siku hiyo, Wizara ya mambo ya nje ya Iraq ililaani mashambulizi yaliyofanywa na baadhi ya waandamanaji dhidi ya ubalozi wa Iran huko Najaf nchini Iraq Jumatano usiku. Imesema lengo la mashambulizi hayo ni kuathiri uhusiano wa kihistoria kati ya Iraq na Iran, na nchi nyingine zenye ubalozi nchini Iraq.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako