Rais Donald Trump wa Marekani amefanya ziara ya ghafla kwenye kituo cha jeshi la Marekani nchini Afghanistan. Hii ni mara ya kwanza kwa rais Trump kufanya ziara nchini Afghanistan, baada ya kukosolewa kutokana na kutotembelea jeshi la Marekani katika maeneo ya vita nje ya nchi kwa karibu miaka miwili tangu alipoingia madarakani. Alitembelea kwa mara ya kwanza jeshi la Marekani nchini Iraq wakati wa sikukuu ya Krismas ya mwaka 2018.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |