Wachezaji 150 wa Gofu wakiwemo kutoka Kenya, Uganda, Malawi, Zambia, Burundi na Rwanda na wenyeji Tanzania wanatarajia kuingia viwanjani katika Mashindano ya Taifa ya Mchezo wa Gofu ya Tanzania Open Mwaka 2019 yanayoanza leo katika Uwanja wa Kili Jijini Arusha. Mwenyekiti wa Chama cha Gofu Tanzania (TGU) Chriss Martin amesema zawadi nono ikiwemo ya gari zitatolewa. Klabu za Tanzania zinazoshiriki mashindano hayo yaliyodhaminiwa na Oryx, Super Doll, Garda word, Coca Cola, Tanfoam na Serengeti, ni Lugalo Golf Club na Dar es Salaam Gymkhana zote za Dar es Salaam, Morogoro Gymkhana, Arusha Gymkhana, Mufindi na Zanzibar sea Cliff.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |