Shirika la ndege la India Air India limerejelea safari zake kati ya Mumbai na Nairobi Kenya baada ya kuzisimamisha kwa miaka 10.
Mkurungezi mkuu wa halmashauri ya utalii nchini Kenya Betty Radier, amesema kurejea kwa huduma za shirika hilo kutasaidia kukuza utalii, biashara na kufungua fursa kwa watu wa pande zote mbili.
Amesema India ni mojawepo wa masoko makubwa ya utalii kwa Kenya, mwaka 2018 kenya ilipokea watalii 125,000 kutoka India.
Shirika hili litafanya safari nne za moja kwa moja kila wiki, Jumanne, Jumatano, Ijumaa na Jumapili.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |