Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Antonio Guterres amemteua Bw. Mark Carney ambaye sasa ni mkuu wa Benki ya Uingereza kuwa mjumbe maalumu anayeshughulikia hatua za kivitendo na mambo ya fedha kwa ajili ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Akiwa mjumbe maalumu Bw. Carney atazingatia utekelezaji kabambe wa hatua za kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa, kuhamasisha fedha za kijamii na binafsi kuchangia juhudi za kutimiza lengo la Mkataba wa Paris wa kudhibiti ongezeko la joto duniani chini ya nyuzi 1.5.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |