• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tamasha la pili filamu la kimataifa la Kisiwa cha Hainan lafunguliwa

    (GMT+08:00) 2019-12-02 19:15:01

    Tamasha la Pili la Kimataifa la Filamu la Kisiwa cha Hainan lililoandaliwa na Shirika Kuu ya Utangazaji la China (CMG) na serikali ya mkoa wa Hainan limefunguliwa jana huko Sanya, mkoani humo.

    Akizungumza katika uzinduzi wa tamasha hilo, Mkuu wa CMG Bw. Shen Haixiong amesema anatarajia waandaaji wa filamu kutoka nchi mbalimbali wataweza kujenga kwa pamoja tamasha hilo liwe jukwaa la mawasiliano, kutoa nguvu na ujuzi kwa maendeleo ya filamu,na kujenga jumuiya ya binadamu yenye mustakabali wa pamoja.

    Naibu katibu wa kamati ya chama ya mkoa wa Hainan Bw. Shen Xiaoming amesema, lengo la tamasha hilo ni "kufanya maonyesho kwa mwaka mzima, kuhusisha kisiwa kizima, na kuwafanya wakazi wote kuyatazama".

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako