• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Bei za vyakula zapanda kutokana na mvua nyingi Rwanda

    (GMT+08:00) 2019-12-02 20:54:15
    Wauzaji bidhaa za chakula rejareja nchini Rwanda wanalalamika kuongezeka kwa bei za chakula kutokana na mvua nyingi katika miezi michache iliyopita.

    Wakulima katika soko la Gikondo,Nyabugogo,na Huye,katika mkoa wa Kusini wameeleza malalamiko yao kuhusu kupanda kwa bei za vyakula.

    Bei za bidhaa za chakula kama vile maharage na choroko zimeongezeka mara mbili kwa kila kilo kutoka Rwf600-800 katika kipindi cha miezi mitano.

    Katika soko la Gikondo maharage kilo mopja yanauzwa Rwf1100 kutoka Rwf500 mapema mwaka huu.

    Vitunguu katika soko la Huye vinauzwa Rwf1400 kwa kilo kutoka Rwf800.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako