Taarifa ya Mkuu wa Wilaya ya Same, Rosemary Senyamule inaeleza kuwa eneo hilo ni mahususi kwa ajili ya kutekeleza shughuli za viwanda na zingine za kiuchumi ili kutoa ajira kwa makundi ya vijana.
Alisema sekta ya viwanda inapewa kipaumbele kwa sasa kwa sababu ya nafasi kubwa iliyonayo katika kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja na kuongeza pato la taifa.
Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya alisema viwanda hivyo vinachangia kuongeza ajira, soko la bidhaa za kilimo kupitia malighafi na mzunguko wenye sura pana katika kukuza uchumi wa nchi.
Hivi karibuni, Mkurungenzi wa Maendeleo ya Teknolojia na Uendelezaji Viwanda wa Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), Mhandisi Emmanuel Saiguran, alikaririwa akisema uanzishaji wa viwanda vidogo utasaidia uchumi kukua na kutoa ajira kwa wingi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |