• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Mamlaka ya Kukusanya Ushuru (KRA)  imelazimika kukanusha madai kwamba ilikuwa na mipango ya kuanza kutoza ushuru kwa wanaopokea mahari.

    (GMT+08:00) 2019-12-06 19:20:27
    Mamlaka hiyo iliandika katika mtandao wa Twitter ikijitetea dhidi ya madai hayo, ambayo tayari yalikuwa yamepingwa vikali na Wakenya.

    Awali, ripoti zilienezwa mitandaoni kuwa KRA ilikuwa imeafikia uamuzi wa kutoza ushuru wa mahari baada ya kushindwa kutimiza kiwango cha ushuru ilichohitajika kukusanya.

    Baadhi ya Wakenya walifahamisha mamlaka hiyo kwamba vijana tayari wamelemewa na maisha, na hivyo hawakuhitaji mzigo mwingine wa ushuru.

    Hata hivyo kuna wengine waliosisitiza kwamba KRA ilikuwa kweli imetoa tangazo hilo, lakini ikabadili nia haraka baada ya kuona hisia za Wakenya. Kwa uhalisia, inaweza kuwa vigumu kwa KRA kutoza ushuru wa mahari, ikizingatiwa kuwa wanaooana hawana mitambo ya kielektroniki (ETR), ambayo hutumika kuweka ithibati ya malipo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako