Msemaji wa Akedemia ya Sayansi ya Ulinzi ya Korea Kaskazini amesema kuwa nchi hiyo tarehe 7 alasiri ilifanya jaribio muhimu kwa mafanikio kwenye kituo cha kurusha satelaiti ya Sohae.
Shirika kuu la habari la Korea Kaskazini leo limenukuu taarifa ya msemaji huyu likisema Akedemia ya Sayansi ya Ulinzi ya Korea Kaskazini iliripoti matokeo ya jaribio hilo kwa kamati kuu ya Chama cha Wafanyakazi cha Korea Kaskazini. Lakini halikutaja habari nyingine kuhusu jaribio hilo.
Taarifa hiyo pia imesema jaribio hilo litafanya kazi muhimu katika kubadilisha wadhifa wa kimkakati wa Korea Kaskazini.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |