Botswana inapanga kutunga hati za kisheria zinazolenga kusimamia matumizi ya dawa za jadi, ili kutambua dawa za jadi na kutambua hadhi mwafaka kwake kwenye dawa za kisasa.
Waziri wa afya wa Botswana Bw. Lemogang Kwape jana huko Francistown alitoa hotuba kwa waganga wa jadi kuwa, dawa mseto zimekua kama aina mbadala ya dawa ikiwemo zile za jadi.
Bw. Kwape amesema matibabu ya dawa mseto ni kuunganisha matibabu ya aina mbalimbali ili kuimarisha afya na maisha. Ameongeza kuwa, maendeleo hayo yanasaidia uponyaji wa jadi na kuongeza ubora matibabu, na kuhakikisha kuwa iko salama na inafaa kwa matumizi ya umma.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |