Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imesema kupitia taarifa kuwa Israel "kuendelea kuongeza hali ya wasiwasi huko Gaza kwa kurusha mabomu dhidi ya vituo vya kijeshi vya Hamas na vikundi vingine vya wapiganaji" ni "hatari" na "hakuwezi kukubalika". Katika mashambulizi yaliyotokea alfajiri ya siku hiyo, ndege za Israel zilishambulia vituo vya kundi la Hamas na vifaa yake huko Gaza, ili kulipiza kisasi makombora matatu yaliyotengenezwa kienyeji yaliyorushwa kusini mwa Israel. Hakuna majeruhi walioripotiwa na pande zote mbili.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |