• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Uganda _Congo. Biashara mpakani yatatizika

    (GMT+08:00) 2019-12-09 18:55:37

    Shughuli za biashara kwenye mpaka wa Mpondwe-Lhubiriha, kati ya Uganda na DR Congo

    zilitatizika pakubwa mno mwishoni mwa wiki jana, kufuati mgomo wa wafanyibiashara kutoka Congo, kwa madai ya ukosefu wa usalama.

    Mgomo huo umeathiri biashara za mpakani, huku wacongo wakikashifu vikosi vya waasi vya ADF kwa kuwaua na kuwanyanya raia wa DR Congo. Vile vile, wafanyibiashara wa Congo kutoka DRC mashariki, mji wa Kasindi ambao unapakana na Mpondwe, walifunga maduka yao kama njia ya kusimama na wenzao walio eneo la Beni, wanaolalamika kuhusu kutolindwa na umoja wa Mataifa dhidi ya mashambulizi. Ikumbukwe kwamba wafanyibiashara wengi wa Congo hununua bidhaa zao nchini Uganda, na hivyo basi mashambulizi haya yamelemaza shughuli hizi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako