Mabondia wa Tanzania wametakiwa kujiandaa vyema kabla ya kwenda kushiriki kwenye mashindano makubwa. Rai hiyo imetolewa baada ya mabondia wa Tanzania Swedi Mohamed na Suleiman Saidi kupigwa kwa knockout katika mapambano ya utangulizi kabla ya pambano la marudiano kati ya Andy Ruiz na Anthony Joshua lililofanyika nchini Saudi Arabia. Katibu mkuu wa Kamisheni ya Ngumi za kulipwa nchini Tanzania Yahya Poli amesema, mabondia wanatakiwa kujiandaa vema kabla ya kukubali pambano ili kuepuka fedheha ya kipigo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |