Mwenyekiti wa klabu ya gofu ya Lugalo nchini Tanzani, Brigedia Jenerali Michael Luwongo amesema, wataanzisha shindano la mchezo huo watakaolipa jina la mfanyabiashara maarufu nchini humo, Ali Mufuruki aliyefariki dunia jumapili nchini Afrika Kusini na kuzikwa jana jijini Dar es Salaam. Amesema lengo la shindano ni kukumbuka mchango wa marehemu Mufuruki katika mchezo huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |