Timu tisa zimethibitisha kushiriki katika michuano ya voliboli ya wanawake ya kabla ya msimu inayaotarajiwa kutimua vumbi Disemba 21 na 22 katika uwanja wa Amahoro. Timu hizo nane ikiwemo timu ya taifa ya Botswana watakuwa wanajiandaa kwa michuano ya mabingwa wa Africa Zone IV. Mashindano hayo yaliyoanzishwa mwaka jana, yanaandaliwa na UTB, ambao pia walikuwa washindi wa michuano ya mwanzo na mabingwa wa ligi mwaka2018/2019. Mamlaka ya Mapato ya Rwanda (RRA) ambao walishindwa mwaka jana katika hatua ya fainali nao pia wamejisajili kushiriki mashindano hayo ya siku mbili.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |