Shirika la ndege la Qatar litakuwa na umiliki wa asilimia 60 ya uwanja wa ndege wa Rwanda unaojengwa hivi sasa kwa gharama ya dola za kimarekani bilioni 1.3. Uwanja huo unatarajiwa kutoa ushindani mkubwa kwa uwan jaw a ndege wa Jomo Kenyatta nchini Kenya. Hatua hiyo inafuatia mapatano kati ya Rwanda na serikali ya Qatar ambayo yataifanya serikali ya Qatar kuwekeza nje ya mji mkuu wa Kigali ambao utakuwa ukiwahudumia wasafiri milioni 14 kila mwaka. Ushirikiano huo unafuatiliwa kwa karibu na shirika la ndege la Kenya ambalo hivi sasa linajikokota kibiashara.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |