Timu ya soka ya wasichana chini ya miaka 17 ya Tanzania Bara ambayo ilianza kwa kishindo mashindano ya kombe la Chalenji, jana ililazimika kutoka sare ya mabao 3 – 3 dhidi ya timu ya Burundi. Kwa matokeo hayo, Tanzania Bara imefikisha alama nne sawa na Kenya, ambayo nayo mapema jana asubuhi ililazimishwa sare ya bao 1 – 1 dhidi ya Eritrea, timu iliyoonyesha kiwango kizuri katika mchezo wote. Mashindano hayo yataendelea tena kesho ambapo Tanzania Bara watakutana na Kenya, huku Burundi ikiwavaa Djibouti na Uganda wakikabiliana na Eritrea.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |