Baada ya uongozi wa klabu ya Yanga kutangaza kuvunja mkataba na mshambuliaji Mnamibia Sadney Urikhob, huku pia ikikiri kulemewa na madeni, hatimaye jana timu hiyo imevunja mkataba na striker wake kutoka Uganda, Juma Balinya. Miongoni mwa wachezaji wanaodaiwa kuandika barua ya kuomba kuvunja mikataba yao katika timu hiyo ni beki Mghana Lamine Moro na David Molinga, raia wa DRC. Lakini uongozi wa Yanga hautaki kuwapoteza wachezaji hao kutokana na kuvutiwa na viwango vyao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |