Mkutano wa kazi za kiuchumi uliofungwa leo umesema, China itaendelea kutekeleza sera tulivu ya kifedha mwakani, na kutatua tatizo la kupata mitaji kwa makampuni binafsi, makampuni madogo na yenye ukubwa wa kati. Mkutano huo pia umesisitiza kuwa China itahamasisha uwekezaji kuingia kwenye sekta za uzalishaji wa kisasa, ujenzi wa maisha ya watu, na miundombinu, na kuinua kiwango cha sekta za uzalishaji na matumizi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |