Klabu za Manchester United na Tottenham Hotspur zimeingia vitani kuwania saini ya mshambuliaji wa timu ya Fenerbahce ya Uturuki, Vedat Muriqi. Mshambuliaji huyo mwenye mabao 10 katika mechi 14 amekuwa akimvutia kocha wa Tottenham, Jose Mourinho na Ole Gunnar Solkjeur wa Manchester United. Lakini pia Muriqi inasemekana anawindwa na klabu ya Bournemouth, na kinachosubiriwa ni klabu yake kuonyesha wapi anaweza kwenda.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |