Serikali ya Ethiopia imepongeza kutambulishwa kwa Jukwaa la Biashara la Kimataifa (eWTP) na kusema litakuwa na nafasi muhimu katika kupata fursa za masoko na kuunganishwa kwa kampuni ndogo na za ukubwa wa kati nchini humo.
Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nchi anayeshughulikia Viwanda na biashara nchini humo Mesganu Arga Moach, ambaye amesisitiza nafasi muhimu wa eWTP, ambayo imekuja baada ya kampuni kubwa ya biashara kupitia mtandao wa internet ya China, Alibaba, na Ethiopia kusaini makubaliano ya awali ya kuanzishwa kwa Jukwaa hilo Novemba 25 mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |