Rais Xi Jinping wa China leo amekutana na Mkuu wa mkoa wa Utawala Maalum wa Hong Kong Bibi Carrie Lam ambaye anatoa ripoti ya kazi mjini Beijing.
Rais Xi amesema, mwaka huu umekuwa kipindi chenye hali ya changamoto na utatanishi kwa Hong Kong tangu irudi China, na serikali kuu ya China inampongeza kwa kazi aliyofanya ya kushikilia kanuni ya "Nchi Moja, Mifumo Miwili", na kutekeleza utawala kwa mujibu wa sheria.
Rais Xi ameongeza kuwa, China inalinda kithabiti mamlaka, usalama na maslahi ya maendeleo ya nchi, kushikilia kithabiti sera ya "Nchi Moja, Mifumo Miwili", na kupinga kithabiti nguvu yoyote ya nje kuingilia kati mambo ya ndani ya Hong Kong. Amewataka watu wa Hong Kong washikamane ili kuhimiza kurejesha tena maendeleo ya mkoa huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |