• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya: Kituo cha data kujengwa katia eneo la mji mpya wa Konza

    (GMT+08:00) 2019-12-16 20:55:01
    Serikali ya Kenya imesema ujenzi wa kituo cha taakwimu cha kisasa kwenye mji mpya wa Konza utakamilika ndani ya miaka mitatu ijayo.

    Mkurugenzi Mtendaji wa mji wa kisasa wa Konza John Tanui, amesema kituo hicho ni sehemu muhimu ya jiji hilo na pia kitakuwa kituo cha data cha kitaifa.

    Alisema kituo hicho cha data kitakuwa muhimu kwa mchakato wa kitaifa wa dijitali na kitatoa jukwaa la kuhifadhi data inayohitajika ili kukuza uchumi.

    Tanui amesema hayo wakati wa uzinduzi wa kituo cha Luban katika chuo kikuu cha Machakos.

    Kituo hicho ni hatua ya kwanza ya ujenzi wa jjumla ya mji wa Konza na kinatarajiwa kufungua nafasi 20,000 za ajira.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako