Akizungumza katika mahafali ya 17 ya Chuo cha Taifa cha Utalii jijini Dar es Salaam, Kanyashu ameitaja mikakati hiyo ni pamoja na kuongeza hifadhi za Taifa, ununuzi wa ndege na kuboresha miundombinu ya vivutio vya utalii.
Amesema serikali pia imeboresha miundombinu kwa kujenga barabara na imenunua ndege za kutosha.
Akieleza umuhimu wa sekta hiyo, Kanyashu amesema mpaka sasa inachangia pato la fedha za kigeni kwa asilimia 25 na asilimia 17.5 ya pato la ndani (GDP).
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |