• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Benki kuu za Afrika Mashariki zimegeukia sera za kuwezesha kupunguza mapato kwa kupunguza viwango vya riba

    (GMT+08:00) 2019-12-17 21:10:32
    Benki kuu za Afrika Mashariki zimegeukia sera za kuwezesha kupunguza mapato kwa kupunguza viwango vya riba na uhifadhi wa fedha (CRR) katika jaribio la kukuza uwekezaji wa kibinafsi na kukuza uchumi.

    Wachumi wanasema mabadiliko ya sera hiyo yanaambatana na hali ya sasa ya ulimwengu ambapo benki kuu zinapunguza viwango vya riba kupiga jeki ukuaji katika hali duni ya uchumi wa Dunia.

    Benki ya Dunia inatarajia ukuaji wa wastani wa pato la Taifa katika nchi za Afrika kupungua hadi asilimia 5.9 mwaka huu kutoka asilimia sita mwaka jana, kwa sababu ya hali ya misukosuko katika masoko ya kimataifa na Kenya, Uganda, na Rwanda kurekodi viwango vya ukuaji wa wastani ikilinganishwa na mwaka jana.

    Uchumi wa Tanzania na Burundi unatarajiwa kukua haraka mwaka huu kuliko mwaka wa 2018, kulingana na taasisi ya Bretton-Woods.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako