• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kilimo kuinua uchumi -Jaber

    (GMT+08:00) 2019-12-18 19:39:26
    Meja Jenerali Ibrahim Jaber, mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Mpito, amethibitisha kwamba serikali iko katika harakati za kukagua sheria za uwekezaji na kutoa sheria mpya inayohimiza mtiririko wa uwekezaji nchini, Sudan.

    Aliwaambia waandishi wa habari, katika Ikulu ya Republican kuwa kilimo kinawakilisha nchi kwa njia ya kipekee ya kutoka kwa mzozo wa sasa wa uchumi.

    Aidha amesema kuna vitisho vya kiuchumi ambavyo lazima vishughulikiwe, kama vile ukosefu wa ajira na biashara haramu, katika mipaka.

    Jaber amesema kuwa serikali inaendelea kusaidia bidhaa za muhimu kama vile ngano, mafuta, na dawa za kuokoa maisha licha ya gharama kubwa ya bidhaa hizi ulimwenguni.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako