Mabasi hayo yalikuwa yakisafiri kutoka Mombasa kuja maeneo ya bara licha ya marufuku iliyowekwa dhidi yao na Mamlaka ya Usalama Barabarani (NTSA) wiki jana.
Kampuni hiyo inadaiwa kupokonywa leseni ya kuhudumu baada ya mabasi yake mawili kugongana eneo la Kiogwani katika barabara kuu Mombasa- Nairobi ambapo watu saba walifariki. Watu wengine 60 walijeruhiwa vibaya katika ajali hiyo iliyotokea mwendo wa saa sita za usiku Jumatano wiki jana.
Aidha Jumanne kulitokea habari za kukanganya kwamba NTSA imeondoa marufuku dhidi ya kampuni hiyo ya Modern Coast na kuhusu mabasi yake kurejelea huduma. Hata hivyo mamlaka hiyo ilikana madai hayo.
Awali kampuni hiyo ilikuwa imesema kwamba NTSA imeirejeshea leseni ya kuhudumu baada ya kukagua mabasi yake.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |