Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Nigeria 'Super Eagles', Gernot Rohr, amesisitiza kikosi hicho kimekosa mvuto kama ilivyokuwa miaka ya nyuma. Rohr ameweka bayana kwasasa Super Eagles imekosa wachezaji wakali kama Nwankwo Kanu na Austin Okocha waliyowahi kutesa miaka ya nyuma. Kocha huyo amesema, hakuna tena wachezaji kama hao, na kuweka wazi kuwa Super Eagles ya sasa imesheheni vijana wengi na wanajitahidi kwa kiwango chao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |