• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya Serikali imetoa onyo kwa  kaunti ambazo hazijalipa bili zao

    (GMT+08:00) 2019-12-20 19:00:25
    Serikali imejitolea kulipa bili zote ambazo bado hazijalipwa kufikia mwezi Machi 2020,hatua ambayo imepatia matumaini wafanyibiashara ambo wanadai mabilioni katika utoji wa huduma na bidhaa kwa ofisi za serikali.

    Waziri wa mambo ya ndani Fred Matiang'i amesema Baraza la Mawaziri lilitengeneza ratiba ya jinsi pesa inayodaiwa na wizara, idara za serikali na mamlaka italipwa.

    Dk Matiang'i ameanika magavana wa kaunti 15 kwa kushindwa kulipa deni zao licha ya kupokea pesa kutoka Hazina.

    Ukaguzi uliofanywa na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa niaba ya Hazina ya Kitaifa mwaka jana ilionyesha kuwa serikali za kitaifa na za kaunti zinadaiwa na wauzaji zaidi ya Sh bilioni 225 zilizo nyuma miaka kadhaa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako