• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Sakata la Zlatan na mashabiki wa Malmo moto waendelea kuwaka, Sanamu lake lakatwa pua na mashabiki hao

    (GMT+08:00) 2019-12-25 18:03:13

    Waharibifu wamekata pua ya sanamu ya gwiji wa soka Zlatan Ibrahimovic nje ya uwanja wa Malmo nchini Sweden. Ni kitendo cha hivi karibuni cha uharibifu kilichoilenga sanamu hiyo tangu itangazwe kwamba Ibrahimovic alikuwa amewekeza katika klabu pinzani mwezi uliopita. Mshambuliaji wa zamani wa Sweden Ibrahimovic ,38, alianza kushiriki katika soka ya kulipwa akiichezea Malmo miaka 20 iliopita lakini baada ya kuonekana kupata mafanikio makubwa mashabiki wa Malmo walitegemea Zlatan akitaka kuwekeza kwenye soka lazima awekeze kwenye timu iliyomlea lakini Zlatan akaenda tofauti na matarajio ya mashabiki ambao walimlea kutoka anaanza mpira na sasa Zlatan amewekeza katika timu mpinzani wa Malmo ambayo ni Hammarby Fotbol.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako