• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • China yasema mkutano wa 8 wa wakuu wa China, Japan na Korea Kusini ni wa kimkakati na wa kuangalia siku zijazo

    (GMT+08:00) 2019-12-25 18:54:26

    Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China Bw. Geng Shuang amesema mkutano wa 8 wa wakuu wa China, Japan na Korea Kusini ni wa kimkakati na wa kuangalia siku zijazo, na umepanga mwelekeo na kuweka msingi wa ushirikiano wa nchi hizo tatu katika miaka 10 ijayo.

    Bw. Geng amesema nchi hizo tatu zimekubaliana kuongeza ushirikiano katika ulinzi wa mazingira, mabadiliko ya hali ya hewa, afya, uzeeni, uvumbuzi, michezo na vijana ili kupanua maslahi ya pamoja. Pia zitashikilia kufungua mlango kwa nje na kulinda kwa pamoja utaratibu wa pande nyingi na biashara huria na kuhimiza kusainiwa mapema kwa Makubaliano ya RCEP na kuongeza kasi ya kufanya mazungumzo kuhusu eneo la biashara huria kati ya China, Japan na Korea Kusini ili kuhimiza kwa pamoja mchakato wa mfungamano wa kiuchumi wa kikanda. Na kuongeza mawasiliano na uratibu kuhusu masuala ya kikanda na kimataifa, kuongoza ushirikiano wa kikanda, kujenga muundo wa ushirikiano wa Asia Mashariki unaokidhi mahitaji ya nchi za kanda hiyo na kuhimiza amani, utulivu, maendeleo na ustawi wa kikanda na wa kimataifa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako