Wizara ya mambo ya ndani ya Iraq imesema raia mmoja ameuawa na wengine wanne wamejeruhiwa katika shambulizi la bomu lililotokea jana karibu na uwanja wa soka mashariki mwa Baghdad. Kikosi cha usalama cha Iraq kimezingira eneo la tukio na kuanza uchunguzi kuhusu tukio hilo. Hadi sasa hakuna kundi lolote lililotangaza kuwajibika na shambulizi hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |