Kocha wa timu ya Cricket ya The Cranes ya Uganda Steve Tikolo amerejea nchini Kenya kusherehekea mzimu huu wa sikukuu, ingawa kibarua chake na Shirikisho la Cricket la Uganda (UCA) kimemalizika. Kocha huyo amesema ameridhika na kazi yake aliyofanya na timu hiyo, na kwa sasa anapumzika na familia na kuangalia mambo mengine. Kuhusu kama yuko tayari kurejea UCA, Tikolo amesema atavuka daraja hilo pindi litakapofika. Tayari timu za Cricket za Zimbabwe, Bangladesh, Oman na Qatar zinamwinda kocha huyo ambaye alianza kuifundisha timu ya The Cranes mwaka 2016.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |