• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • SOKA: Yanga yapania tatu za Prisons

    (GMT+08:00) 2019-12-26 17:06:39

    Licha ya matokeo ya sare tasa waliyoyapata katika mechi yao dhidi ya Mbeya City iliyochezwa kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine, jijini Mbeya, Kaimu Kocha Mkuu wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa amewatoa hofu mashabiki wa timu hiyo kuelekea mchezo wao dhidi ya Tanzania Prisons. Yanga itashuka tena uwanjani hapo kesho ijumaa kupambana na Tanzania Prisons iliyoko nafasi ya nne katika mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara ambayo inatarajiwa kuwa mechi ngumu zaidi. Hata hivyo Mkwasa amesema ana uhakika kuwa katika mechi hiyo timu yake itafanya vizuri kama hali ya uwanja itakuwa rafiki.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako