Zikiwa zimesalia siku chache kabla ya watani wa jadi kukutana kwa mara ya kwanza katika msimu huu wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Kocha Msaidizi wa Simba Selemani Matola amesema kuwa bado kikosi chake hakijaanza kuufikiria mchezo huo utakaochezwa Januari 4 mwakani. Matola amesema kwa sasa nguvu na akili zao ziko katika kuhakikisha wanashinda mechi mbili zilizo mbele yao, dhidi ya KMC FC hapo kesho na Desemba 31, watachuana na Ndanda FC. Matola amesema mechi zote za Ligi Kuu ni muhimu, na ili timu iweze kutwaa ubingwa, inatakiwa kukusanya point nyingi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |