Katika kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Magufuli na Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan, Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (Brela) wamefanya bonanza la michezo kwa vikundi 48 vya mpira wa miguu likiwa na lengo wa kujenga afya na kuimarisha uhusiano baina ya wafanyabiashara. Bonanza hilo pia lilikuwa na lengo la kuwaelezea umuhimu wa bima ya afya kwa madereva wa bodaboda na wananchi kwa ujumla. Bonanza hilo lilihudhuriwa na Mwenyekiti wa Bodi wa NHIF Anna Makinda ambaye alikuwa mgeni rasmi, limefanikiwa kwa asilimi 100 kwa kuweza kufikisha malengo yake.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |