Azam FC ilishindwa kutamba mbele ya Coastal Union baada ya kucharazwa bao 1 – 0 kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliochezwa katika Uwanja wa Mkwakwani, Tanga. Ushindi wa wenyeji Coastal Union ulipatikana kwa bao pekee lililowekwa kimiani na mchezaji wake Haji Ugando na kuinyamazisha Azam ambayo haikuweza kufurukuta muda mote wa mchezo. Kwa matokeo hayo, Azam inaendelea kubaki katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi hiyo ikiwa na point 20 sawa na Tanzania Prisons inayoshika nafasi ya nne na Costal imepanda toka nafasi ya 11 hadi nafasi ya tano.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |